WATU wawili wakazi wa Kijiji cha Nyamtukuza Wilaya ya
Kibondo mkoani Kigoma, wameuawa baada ya kupigwa na wananchi wenye hasira
wakituhumiwa kuiba mbuzi wawili wenye thamani ya Sh 40,000.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Fraiser Kashai aliwataja
waliouawa kuwa ni Nongo Bufinkri (36) na Azimio Muhabwa ambao waliiba mbuzi
mali ya Sibalina John na waliuawa juzi mchana kijiji hapo.
Hata hivyo, Kamanda Kashai alisema hadi sasa hakuna mtu
yeyote aliyekamatwa juu ya mauaji hayo ambapo mtuhumiwa mmoja alifanikiwa
kukimbia kabla ya wenzake kukutwa na mauti.
Katika tukio lingine, kamanda huyo alisema mkulima mkazi wa
kijiji cha Kazuramimba Wilaya ya Uvinza, Stephano Muhunzi (70), ameuawa kwa kukatwakatwa
mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake baada ya kuvamiwa na watu wanaosadikiwa
kuwa ni majambazi.
Alisema katika tukio hilo, watu watano walivamiwa nyumbani
kwa Muhunzi majira ya mchana na baada ya kumjeruhi vibaya mwilini waliondoka na
kondoo sita wenye thamani ya Sh 300,000.
No comments:
Post a Comment