SHEHE wa Wilaya ya Kigoma, Ibrahim Kabeke amefariki dunia
baada ya kuugua kwa kipindi kirefu akisumbuliwa na kupanda na kushuka kwa
shinikizo la damu.
Katibu wa Baraza Kuu la Waislamu (Bakwata) Mkoa Kigoma,
Moshi Guoguo alisema mjini hapa jana kwamba Kabeke alifariki dunia juzi jioni
nyumbani kwake Ujiji mjini Kigoma.
Guoguo alisema kuwa alifariki nyumbani kwake ambapo alikuwa
akiugulia baada ya kuwa amepata matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando,
Mwanza.
Alisema kuwa taratibu za mazishi zinafanyika nyumbani kwake
mtaa wa Kabondo mjini hapa. Katibu huyo alisema Shehe Kabeke pia alikuwa
akisumbuliwa na sononeko la moyo kutokana na mfululizo wa vifo vya watoto wake.
Kwa mujibu wa Guoguo, mmoja wa watoto alikuwa akifanya kazi
katika benki nchini na mwingine alikuwa Mhandisi wa Shirika la Reli na
walifariki wakifuatana kwa kipindi kifupi.
No comments:
Post a Comment