Karibu kwenye Blog ya Kijamii ya Kigoma yetu kwa habari na matangazo kwa bei nafuu sana. Tunakalibisha maoni, ushauri na habari zako ili tuijenge Tanzania kwa pamoja.

Saturday, October 27, 2012

Hii ndiyo hali ya ukataji tiketi Mkoani Kigoma




Kwa Waziri mwenye dhamana na wadau wote:
 
Huu ndio utaratibu unaotumika kukata tiketi za treni ya abiria mkoani kigoma. ni utaratibu uliojaa udhalilishaji na hali zote zisizo za kiubinadamu. foleni huwa ndefu sana na huuzwa tiketi chache sana na wananchi kutangaziwa kuwa zimekwisha. hivyo inawabidi watu kulala station kigoma wakipigwa na baridi huku wakiliwa na mbu pia ili kuwahi foleni hiyo waweza pata tiketi kihalali na kukamilisha safari zao. kinachosikitisha zaidi ni kuwa tiketi hizo hizo huendelea kuuzwa nje kidogo ya ofisi za TRL kwa bei kubwa.

Imekuwa ni biashara ya Kawaida kabisa mkoani hapo. tunahitaji utaratibu wa booking urudi ili kutoa fursa ya mtu kufika pale kwa nafasi yake badala ya kupanga foleni ndefu ka watumwa sokoni. pili, walanganguzi wa tiketi ukomeshwe mara moja. NATAMBUA kuwa mnaweza yakamilisha hayo mkiamua...



 
Imetoka kwa Mdau John N Bakunda

No comments: