Karibu kwenye Blog ya Kijamii ya Kigoma yetu kwa habari na matangazo kwa bei nafuu sana. Tunakalibisha maoni, ushauri na habari zako ili tuijenge Tanzania kwa pamoja.

Sunday, September 30, 2012

Watu 473 wafunga kizazi Kigoma


Mganga Mkuu wa Mkoa Kigoma, Dr.Leonald Subi
 JUMLA ya watu 473 mkoani Kigoma wakiwemo wanaume 23 wamejitokeza kupatiwa huduma ya kufunga kikazi katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita ikiwa ni katika mkakati wa utekelezaji wa uzazi wa mpango na kufuata nyota ya kijani.

Mganga Mkuu wa Mkoa Kigoma, Leonald Subi alisema hayo wakati wa uzinduzi wa mradi wa huduma za mkoba za uzazi wa mpango na upimaji wa hiari wa Virusi Vya Ukimwi .

Mganga huyo alisema kuwa kwa idadi hiyo ya watu hayo ni mafanikio makubwa tangu kuanza kutekelezwa kwa mpango huo mwezi Julai mwaka huu hasa kwa kuzingatia historia na utamaduni wa wananchi wa Mkoa Kigoma.

Subi alisema kuwa Mkoa wa Kigoma kwa miaka mingi umekuwa na takwimu za juu za watoto wanaozaliwa huku familia nyingi za wananchi wa mkoa huo wakiwa wanazaa bila kujali uzazi wa mpango jambo ambalo limechangia umasikini kwa familia nyingi mkoani humo.

Awali Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Marie Stops Tanzania, Zawadi Athanas alisema kuwa uzinduzi wa mradi huo kwa Mkoa Kigoma na sehemu ya utekelezaji wa mradi wa miaka minne kwa mikoa 26 ambayo itafikiwa na huduma hizo za mkoba za uzazi wa mpango.

Akizindua mradi huo Mkuu wa Mkoa Kigoma, Issa Machibya alitoa wito kwa jamii ya mkoa huo kufuata njia za uzazi wa mpango zilizokubaliwa na wataalamu kwani kufanya hivyo kutasaidia kuinua uchumi wa familia nchini .

Mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa bado Mkoa Kigoma una takwimu za chini za watu wanaojitokeza kufuata uzazi wa mpango na kueleza kushangazwa na kuongezeka kwa takwimu za wanawake walioolewa kuendelea kushindwa kupata huduma za uzazi wa mpango.

No comments: