Karibu kwenye Blog ya Kijamii ya Kigoma yetu kwa habari na matangazo kwa bei nafuu sana. Tunakalibisha maoni, ushauri na habari zako ili tuijenge Tanzania kwa pamoja.

Monday, August 6, 2012

Vifo vya wajawazito bado ni tatizo kubwa Kigoma

MKOA wa Kigoma bado unakabiliwa na changamoto kubwa ya kuendelea kuwepo kwa vifo vya wajawazito na watoto chini ya miaka mitano kutokana na wajawazito wengi kujifungulia nyumbani.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Dk Leonard Sumbi alisema hayo wakati wa mkutano wa wadau wa Sekta ya Afya mkoani humo uliokuwa ukijadili mkakati wa kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto chini ya miaka mitano.

Dk Maginga alisema kuwa zaidi ya asilimia 42 ya wanawake wajawazito mkoani humo bado wanajifungulia majumbani na watoto au wanawake hao hufariki dunia kutokana na kuchelewa kufikishwa hospitalini wanapopatwa na matatizo wakati wa kujifungua.

Sambamba na hilo, alisema kuwa suala la uchache wa watumishi katika Sekta ya Afya na miundombinu duni ya usafiri katika maeneo ya mbali vijijini kufika katika maeneo ya utoaji huduma za afya ni miongoni mwa changamoto zinazochangia katika ongezeko la vifo hivyo.

Hata hivyo, alisema kuwa kuanzishwa kwa huduma za upasuaji katika vituo 12 vya afya mkoani humo kulikofanywa kupitia ufadhili wa taasisi ya World Lung Foundation kumesaidia katika kukabiliana na vifo vya wanawake wakati wa kujifungua kutokana na kufanyiwa upasuaji mdogo kwenye vituo hivyo.

No comments: