HALMASHAURI ya Manispaa ya Kigoma Ujiji inatarajia kuendesha
bonanza la michezo litakalofanyika leo kwenye Viwanja vya Mwanga Community
Centre mjini Kigoma likiwa na nia ya kuhamasisha Sensa ya Watu na Makazi
inayotarajiwa kuanza Jumapili wiki hii.
Akizungumza mjini Kigoma na waandishi wa habari, Mkurugenzi
wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Alfred Luanda amesema moja ya sababu kuu za kuwepo
kwa bonanza hilo
ni kuwapa nafasi watu ambao hawajapata elimu kuhusu sensa kupitia vyombo vya
habari na maeneo mengine kupata ujumbe na kuweza kufanikisha shughuli hiyo.
Luanda amesema bonanza hilo litafanyika kwenye Viwanja vya
Mwanga Community Centre mjini Kigoma mahali ambapo wadau na watu mbalimbali
watafika kwa urahisi, lakini pia ni eneo ambalo lina msongamano mkubwa wa watu
na ujumbe unaweza kusambaa kwa urahisi.
No comments:
Post a Comment