Karibu kwenye Blog ya Kijamii ya Kigoma yetu kwa habari na matangazo kwa bei nafuu sana. Tunakalibisha maoni, ushauri na habari zako ili tuijenge Tanzania kwa pamoja.

Wednesday, July 25, 2012

Waziri atangaza kuwafukuza watendaji wabovu

Mh.Aggrey Mwanri

NAIBU Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Aggrey Mwanri ametangaza kuwafukuza kazi watendaji wabovu na wanaokiuka maadili ya kazi mkoani hapa.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mwanri alisema anazo taarifa kwamba wapo baadhi ya wafanyakazi katika baadhi ya vituo vya afya, zahanati na hospitali mkoani Kigoma ambao wamekuwa wakiwataka wanaojifungua kutoa fedha kwa ajili ya nyembe na glovu wakati wa kujifungua.

Nimeisikia kero hii kwamba ipo pia kwenye hospitali zetu hapa Kigoma, sasa nawaambieni tafadhalini sana acheni tabia hii mara moja, na ninatangaza mbele ya kadamnasi hapa kwamba, tutakayempata anakiuka taratibu zetu nitamshukia mzima mzima na kumfukuza kazi mara moja", alisema Mwanri.

Mwanri alisema tabia hiyo ni kinyume na utaratibu na maagizo ya Serikali, kwa kuwa wajawazito, wazee, watoto na wenye magonjwa sugu hawapaswi kutozwa malipo wakati wa kupatiwa matibabu.

Alisema, Serikali imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya kuhudumiwa watu wa kada hiyo bure.
Sasa haingii akilini anapotokea mtumishi wa umma anamdai fedha mwananchi mwenye fursa ya kuhudumiwa bure,” alisema.

Akizungumzia kero ya wauza maandazi na mchicha kutozwa ushuru, Mwanri alizitaka halmashauri za miji hapa nchini kote ikiwemo ya Mji wa Kigoma, kuacha mara moja akisisitiza siyo wafanyabiashara wanaopaswa kutozwa ushuru.

Akizungumzia kuhusu kupandishwa ushuru kwa wachuuzi mkoani Kigoma kutoka Sh 200 hadi 300, Mwanri alisema, kiwango kilichopandishwa kinaonesha kuwa mzigo mkubwa kwa wafanyabiashara hivyo ameshauri uongozi wa Halmashauri ukutane na kutafuta namna nzuri itakayoweza kuweka viwango nafuu.

Ataja faida za Serikali kujiunga na Azaki Na Shadrack Sagati OFISI ya Rais (Mejementi ya Utumishi wa Umma) imesema kuwa zipo faida kubwa ambazo zitapatikana iwapo Serikali itashirikiana na asasi zisizokuwa za kiserikali (Azaki) katika kuimarisha majadiliano juu ya ubora wa huduma zinazotolewa na Serikali kwa watumishi.

Katibu Mkuu Utumishi, George Yambesi katika hotuba yake iliyosomwa na Naibu Katibu Mkuu, Hab Mkwizu alitaja baadhi ya faida hizo kuwa ni pamoja na kufanya maamuzi yenye tija na kwa wakati muafaka na kutathmini utendaji kazi na watumishi wa umma kupitia maoni ya wananchi wanaopokea huduma kutoka kwenye ofisi za Serikali.

 Alikuwa anafungua mkutano wa ushirikiano baina ya Serikali na Azaki katika kuimarisha utoaji huduma kwa umma. Mkutano huo unashirikisha baadhi ya maofisa habari wa Serikali, wahariri wa vyombo vya habari na wawakilishi kutoka kwenye asasi zisizokuwa za kiserikali.

Yambesi alisema utaratibu huo pia utasaidia Serikali kuimarisha uwajibikaji na uwazi katika utoaji wa uamuzi, hususan katika sera zinazohusu huduma kwa jamii kwa kuwa Serikali itakuwa na uwezo wa kukosoa na kuboresha pale ambapo sera hizo hazitatekelezwa ipasayo kulingana na maoni ya wananchi.

Katibu mkuu huyo alisema utaratibu wa ushirikiano baina ya Serikali na Azaki utasaidia kuongeza uelewa wa masuala ya sera na maendeleo yanayotekelezwa na Serikali na kuimarisha ushiriki wa wananchi katika mchakato wa demokrasia na utawala bora.

No comments: