BAADHI ya maduka ya kuuza dawa muhimu mjini Kigoma yamedaiwa kukiuka 
kanuni na utaratibu wa utendaji wake kwa kuuza dawa za kutibu ugonjwa wa
 kifua kikuu (TB) kiholela, jambo ambalo ni kosa kisheria. 
Uchunguzi
 uliofanywa na Asasi ya Mapambano ya Kifua Kikuu na Ukimwi Tanzania 
(Mkuta),  mkoani Kigoma umebaini kuwepo kwa dawa hizo kwenye maduka ya 
dawa baridi ya jumla na rejareja, hivyo kukiuka sheria inayoelekeza dawa
 hizo zitolewe bure katika hospitali, vituo vya afya na zahanati 
zilizoteuliwa rasmi na mamlaka husika. 
Mratibu wa Asasi ya MKUTA
 Mkoa wa Kigoma, Maulidi Ntahondi alibainisha ukiukwaji huo wa sheria 
akitaja maeoneo husika kuwa ni Kigoma mjini, Bangwe, Gungu na Mwanga na 
kwamba maelekezo yanayotolewa na wahudumu wa maduka hayo kuhusu utumiaji
 dawa hizo  yanatofautiana.
 
Aliongeza kuwa dawa hizo huuzwa kwa Sh10,000 kwa boksi moja ambapo pia dozi moja ya vidonge ishirini huuzwa kwa Sh4000.
Alipotafutwa
 kuzungumzia suala hilo, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dk Yakayashi 
Macrice alisema kuuza dawa za kutibu TB kwenye maduka hayo binafsi ni 
kosa kisheria na kwamba wahusika wanastahili kukamatwa na kufikishwa 
mahakamani.
Alisema kuwa dawa hizo zinatolewa na Bohari Kuu ya 
Dawa ya Serikali na zinapaswa kutolewa bure kwa wagonjwa wa TB na kwamba
 ni lazima zitolewe katika vituo vya afya, hospitali au kwenye zahanati 
maalumu zilizoteuliwa kulingana na jiografia ya wilaya husika zikiwa na 
wataalamu wa afya. 
Alimuagiza Mfamasia Mkuu wa Mkoa wa Kigoma 
kuhakikisha kuwa wote wanaouza dawa hizo kwenye maduka binasfi 
wanakamatwa na kufikishwa mbele ya sheria.
Baadhi ya watumishi wa
 maduka binafsi ya dawa yanayouza dawa hizo bila kufafanua walieleza 
kuwa dawa hizo za TB huuzwa kwa kuwa zina matumizi tofauti na kutibu 
ugonjwa huo 
No comments:
Post a Comment