Karibu kwenye Blog ya Kijamii ya Kigoma yetu kwa habari na matangazo kwa bei nafuu sana. Tunakalibisha maoni, ushauri na habari zako ili tuijenge Tanzania kwa pamoja.

Wednesday, June 27, 2012

Kigoma hoi kwa Ruvuma

TIMU ya Ruvuma imeanza vema mashindano ya Copa Coca-Cola yanayoshirikisha vijana chini ya umri wa miaka 17 ngazi ya Taifa baada ya kuwalaza mabingwa watetezi Kigoma mabao 2-0 katika mchezo wa kundi A uliofanyika kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

Kigoma ambao walianza mashindano kwa kasi na kuwatandika Lindi mabao 2-0 katika mechi ya ufunguzi mwishoni mwa wiki iliyopita, jana walishindwa kufurukuta mbele ya Ruvuma na kuruhusu bao katika kila kipindi.

Mabao yote ya washindi yalifungwa na mshambuliaji Edward Songo katika dakika ya 34 na 84. Katika mechi nyingine za jana, Tanga na Morogoro walitoka sare ya mabao 3-3 kwenye mchezo uliofanyika Uwanja wa Tanganyika Packers, Kawe jijini.

Mkoani Pwani, Mara waliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Temeke Uwanja wa Nyumbu, wakati Kagera walilala kwa bao 1-0 mbele ya Kilimanjaro katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Tamco.

Wakati huohuo, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetangaza dau kwa wapigapicha za magazeti watakaoripoti mashindano ya Copa Coca-Cola yanayoendelea kwenye mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.

Mashindano hayo yanayodhaminiwa na Kampuni ya Coca-Cola na kushirikisha mikoa 28 yanafanyika Viwanja vya Tanganyika Packers, Kumbukumbu ya Karume mkoani Dar es Salaam, na Viwanja vya Tamco na Nyumbu mkoani Pwani.

Ofisa Habari wa TFF, Boniface Mwabura alithibitisha taarifa hizo na kusema zawadi ya Sh 250,000 itatolewa kwa picha bora katika maeneo matatu.

Aliyataja maeneo hayo kuwa ni picha ya kitendo (action picture), haki (fair play picture) na mpigapicha ambaye ameripoti matukio mengi ya mashindano

No comments: