Karibu kwenye Blog ya Kijamii ya Kigoma yetu kwa habari na matangazo kwa bei nafuu sana. Tunakalibisha maoni, ushauri na habari zako ili tuijenge Tanzania kwa pamoja.

Wednesday, May 30, 2012

Wakuu wa wilaya wapya Kigoma waahidi kusimamia maendeleo

Mkuu wa mkoa wa Kigoma, Luteni kanali mstaafu Issa Machibya
 
Wakuu wa wilaya mbalimbali mkoani Kigoma wamekula viapo vya utii na kuahidi kushirikiana na wananchi katika kusimamia  kikamilifu maswala ya ulinzi na usalama, utekelezaji wa  miundo mbinu ya huduma za jamii zikiwamo za elimu, afya na utekelezaji wa miradi ya kilimo na uvuvi.
 
Wakuu hao wa wilaya sita tofauti,  wametoa ahadi hizo kwa nyakati tofauti baada ya kula kiapo cha utumishi wao mbele ya mkuu wa mkoa wa Kigoma Luteni kanali mstaafu Issa  Machibya.
Waliokula kiapo cha utii wa utumishi  ni pamoja na mkuu wa wilaya ya Kasulu Dany Makanga ambaye kabla ya kuhamishiwa kituo kipya cha kazi alikuwa ni mkuu wa wilaya ya Kibondo na amekuwa akikaimu wilaya za  Buhigwe, Kakonko na Kasulu yenyewe.

Wengine waliokula kiapo cha utii ni pamoja na mkuu wa wilaya mpya ya Uvinza Hadijah Nyembo, Venance Mwamoto ambaye ni mkuu wa wilaya ya Kibondo na Gishule Charles ambaye atakuwa katika wilaya mpya ya Buhigwe.
Kanali Cosmas Kayombo  yeye amekula kiapo cha kuwatumikia wananchi wa wilaya mpya ya  Kakonko, wakati Rajabu Maneno ameapa kuwa mkuu wa wilaya ya Kigoma.

No comments: