Wananchi
na viongozi mkoani Kigoma wametahadharishwa kuwa macho na wahamiaji
haramu na wageni toka nje ya nchi wakati wa kutoa maoni ya katiba mpya.
Tahadhari hiyo imetolewa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Danh Makanga
katika mkutano wa hadhara wa uhamasishaji wananchi kujitokeza kwa wingi
wakati ukifika kutoa maoni .
Amesema
kufuatia kuwepo kwa maelfu ya wahamiaji haramu katika mkoa wa Kigoma na
mwingiliano mkubwa wa wananchi toka Burundi na Kongo DRC, wananchi
wanatakiwa kuhakikisha raia hao wa nchi jirani hawapati nafasi ya
kuchangia kwa kuwa ni kinyume cha sheria.
“Nawaomba
sana, kama mnavyojua tunajua Warundi wengi na Wakongo hapa kwetu, wamo
vijijini mwetu na mijini, sasa wakati ukifika tuwe makini wasipate
nafasi kwani kwa kufanya hivyo tutakuwa tumenusuru kupata maoni ya nchi
zao kwenye katika yetu,” alisema.
Alisema
mwingiliano mkubwa wa raia toka nchi jirani kuna uwezekano mkubwa kwa
wageni kujipenyeza na kutoa maoni katika tume, hivyo ni jukumu la kila
Mtanzania kuhakikisha kuwa wageni hawapati fursa hiyo kwani wanaweza
kupendekeza vitu ambavyo si mahitaji ya Watanzania.
Mkoa
wa Kigoma una zaidi ya wahamiaji haramu 1000 toka Burundi na Kongo
(DRC) wanaoishi kinyume cha sheria katika maeneo mbalimbali mkoani hapa .
Naye
Mbunge wa viti maalum CCM kupitia mkoa wa Tabora, Munde Tambwe, amesema
fursa ya wananchi kutoa maoni ikitumiwa vizuri itawezesha masuala
mbalimbali yanayolalamikiwa kupatiwa ufumbuzi.
“Wananchi
wenzangu tusiwe watu wa kulalamika tu , fursa inakuja tuotumie vizuri
kuhakikisha tunayoyataka yanakuwemo na hakuna namna ya kuhakikisha
tunayoyataka yanakuwemo kama kushiriki kutoa maoni tume itakapopita,’’
alisema.
No comments:
Post a Comment