uduma
za safari za treni za abiria za Kampuni ya Reli Tanzania -TRL kutoka
Dar es Salaam kwenda Kigoma zinatarajiwa kuanza keshokutwa ambapo abiria
wanaweza kuanza kukata tiketi hii leo katika stesheni husika.
Kwa
mujibu wa taarifa iliyotolewa na TRL, kuanza tena kwa huduma hiyo
kumetokana na kukamilisha kazi ya ukarabati ambayo imewezesha treni za
mizigo zipatazo 10 kutoka na kwenda bara kupita eneo la Godegode mkoani
Dodoma.
Hata
hivyo mafundi wa TRL bado wanaendelea na kazi ya kuimarisha tuta la
reli katika maeneo mawili korofi eneo la Stesheni ya Godegode ambayo
hukumbwa na mafuriko na kusababisha reli kuharibika.
Huduma
za treni zilisimamishwa Januari 07, 2012 baada ya kutokea uharibifu
mkubwa katika eneo la stesheni ya Godegode kufuatia mafuriko yaliyokumba
eneo hilo baada ya mvua kubwa kunyesha katika mikoa ya Morogoro, Iringa
na Dodoma.
No comments:
Post a Comment