Familia
tano za ukoo mmoja kutoka kijiji cha Nnyegera katika Wilaya ya Kasulu
mkoani kigoma, zimekimbia kijiji hicho na kuhamia ofisi ya Mkuu wa
Wilaya ya Kasulu, baada ya ndugu zao wawili kuuawa na wananchi na wao
kuchomewa nyumba na mali zao kwa tuhuma za uhalifu na uhasama na
wananchi.
Familia
hizo kutoka ukoo wa Chubwa zenye watu wazima 45 na watoto 35, zimepiga
kambi ofisi ya DC na kulala nje kwa zaidi ya wiki mbili zikiomba
hifadhi.
Kiongozi
wa familia hiyo, Edward Chubwa, alisema wamelazimika kukimbia baada ya
serikali ya kijiji na wananchi kuwatuhumu na kuwaua ndugu zao kikatili
mwishoni mwa mwaka jana kwa madai ya wizi, ambayo alisema sio ya kweli.
Alisema
matukio hayo yaliyotokea kati ya Septemba na Disemba mwaka jana,
yalifuatiwa na vitisho, kuchomewa nyumba na mali zao na kwamba kutokana
na hali hiyo walilazimika kukimbilia polisi na baadaye ofisi ya DC ili
kunusuru maisha yao na kwamba watoto 13 waliokuwa wakisoma kijijini hapo
wamekatisha masomo.
Walidai
kuwa ndugu yao, Method Chubwa, aliuawa na wananchi kwa kuchomwa moto
kwa madai ya ujambazi Aprili 2011, madai ambayo alisema si ya kweli na
kwamba baada ya mauaji hayo baadhi ya wananchi walikikimbia kijiji hicho
kuhofia kukamatwa.
Hata
hivyo, alisema walianza kurudi kijijini baadaye ndipo polisi
ilipowakamata watu saba, hali iliyozua uhasama mkubwa kijijini baina ya
familia hiyo na jamii na polisi kulazimika ikuweka kambi kijijini hapo.
Hata
hivyo vitisho viliendelea na Oktoba na Desemba, kundi la wananchi
lilivamia nyumba ya ndugu yao Samson Chubwa kwa madai kuwa ana vitu vya
wizi na kuanza kumpiga hadi akapoteza maisha.
Amesema kutokana na kutengwa na wananchi kijiji ni walilazimika kukimbilia kituo cha polisi kwa usalama zaidi.
Kaimu
Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Dahn Makanga, ambaye pia, alisema polisi
wanaendelea na uchunguzi na kwamba watu kadhaa wananshikiliwa kuhusiana
na matukio hayo.
Amesema kwa hali ilivyo kijijini hapo, isingewezekana wananchi hao kuishi kwa amani hivyo serikali itawatafutia sehemu salama.
Amesema
Serikali imekuwa ikiwahudumia kwa chakula na malazi kwa siku zote,
lakini wiki iliyopita walikubaliana na familia hizo baada ya kuwapa
magodoro na vitu vya kuanzia maisha pamoja na Sh.125,000 kwa kila
familia na nyumba ya kukaa kwa muda nje ya mji wa Kasulu, lakini
waligoma na kuendelea kuishi nje ya ofisi ya DC.
Makanga,
amebainisha kuwa kutokana na hali hiyo, familia hizo zitahamishiwa kwa
muda katika kambi ya wakimbizi wa Burundi ya Mtabila wakati serikali
ikijiandaa kuwapeleka katika moja ya vijiji vya wilaya hiyo kuanza
maisha mapya.
Alisema
wakiwa katika kambi hiyo, watahudumiwa na serikali na kwamba baada ya
miezi mine watapelekwa kwenye kijiji kimojawapo na kupewa ardhi na
viwanja ili waishi huko.
No comments:
Post a Comment