Karibu kwenye Blog ya Kijamii ya Kigoma yetu kwa habari na matangazo kwa bei nafuu sana. Tunakalibisha maoni, ushauri na habari zako ili tuijenge Tanzania kwa pamoja.

Tuesday, January 3, 2012

Kigoma yakabiliwa na uhaba wa maji

MJI wa Kigoma Ujiji na vitongoji vyake hauna huduma ya maji inayotolewa na Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Kigoma Ujiji (KUWASA) kwa zaidi ya siku nne sasa kutokana na kukatiwa umeme katika mitambo yake ya kusukumia maji.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kuwasa, Saimon Lupuga amethibitisha kutokuwepo kwa huduma
hiyo tangu mwanzoni mwa wiki hii na kusema kuwa hali hiyo inatokana na kukatwa kwa huduma ya umeme katika mitambo yake ya kusukumia maji iliyopo Bangwe mjini Kigoma.

Lupuga alisema kuwa kitendo cha mamlaka yake kukatiwa maji kwa siku ya nne kimetokana na kudaiwa na Shirika la Umeme (TANESCO) Mkoa Kigoma kiasi cha Sh milioni 321 ikiwa ni madai ya matumizi ya umeme iliokuwa ukitolewa kwenye mitambo hiyo ya kusukumia maji.

Mkurugenzi huyo amekiri kuwepo kwa deni la muda mrefu ambalo Tanesco inaidai Kuwasa na
kwamba deni hilo lilirithiwa na mamlaka hiyo kutoka iliyokuwa Idara ya Maji.

Mbali na kuendelea kwa deni hilo, pia Mkurugenzi huyo alikiri kuwa deni limeongezeka kutokana na makusanyo yanayofanywa na mamlaka hiyo kutokidhi ulipaji wa matumizi ya umeme wanayotumia kwa mwezi.

Akizungumzia hali hiyo, Meneja wa Tanesco Mkoa wa Kigoma, Cleophasi Tibaijuka alisema
kuwa shirika hilo linajiendesha kibiashara na limekuwa likigawia Kuwasa umeme wenye
thamani kati ya Sh milioni 43 na 44 kila mwezi.

Tibaijuka alisema kuwa wamekuwa wakitoa kipaumbele kwa mitambo ya kusukuma maji ya
Kuwasa kutokana na unyeti wa huduma hiyo kwa jamii lakini ulipaji wa deni hilo kutokana na matumizi ya umeme wanaotumia umekuwa wa kusuasua sana.

No comments: