Karibu kwenye Blog ya Kijamii ya Kigoma yetu kwa habari na matangazo kwa bei nafuu sana. Tunakalibisha maoni, ushauri na habari zako ili tuijenge Tanzania kwa pamoja.

Tuesday, October 11, 2011

RC Kigoma aagiza sheria kusimamiwa kikamilifu

Mkuu wa mkoa wa Kigoma Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya ametembelea maeneo ya kijiji cha Munanila wilayani Kasulu na  kijiji cha Mukarazi wilayani Kibondo vilivyopo mpakani mwa Tanzania na Burundi na kuvitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha kuwa hakuna uvunjaji wowote wa sheria unaotokea  katika maeneo ya mpakani.
 
Mkuu huyo wa Mkoa wa Kigoma  ameongeza kuwa wakati vyombo vya ulinzi na usalama vikiendelea kutekeleza majukumu yake  hayo, nayo mamlaka ya mapato katika maeneo ya mpakani inatakiwa kusimamia kikamilifu ukusanyaji wa mapato kwa kutoza kodi bidhaa zote zinazostahili  kutozwa kodi, iwe zinaingizwa nchini ama kwenda nchi jirani.

No comments: