Karibu kwenye Blog ya Kijamii ya Kigoma yetu kwa habari na matangazo kwa bei nafuu sana. Tunakalibisha maoni, ushauri na habari zako ili tuijenge Tanzania kwa pamoja.

Wednesday, June 19, 2013

Mwanamke aliyesalimisha SMG Kigoma azawadiwa fedha

SERIKALI wilaya ya Kibondo imemzawadia fedha taslimu kiasi cha shilingi 50,000 mwanamke mmoja mkulima na mkazi wa kijiji cha Kitahana wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma kwa kuisalimisha polisi bunduki aina ya SMG aliyoiokota.



Mkuu wa Wilaya ya Kibondo, Venance Mwamotto ambaye ni Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo alikabidhi fedha hizo kwa mwanamke huyo aliyejulikana kwa jina la Ericca Josamu.



Akizungumza baada ya kukabidhi fedha hizo mkuu huyo wa wilaya Kibondo, alisema kuwa kitendo kilichofanywa na mwanamke huyo kinapaswa kupongezwa kwani licha ya kuiokota na kuisalimisha lakini angeweza kuiacha na baadaye kuokotwa na watu wenye dhamira mbaya.



Mwamoto alisema kuwa fedha iliyotolewa ni kidogo mno, lakini imetolewa ikiwa ni kuwapa hamasa hata watu wengine watakaookota silaha yoyote ile aweze kupeleka katika vyombo husika na atapewa zawadi kama huyo mwanamke aliyefanya hivyo.



Ericca Josamu aliliambia gazeti hili kuwa Jumamosi ya wiki iliyopita majira ya asubuhi wakati akielekea shambani kwake mara aliona mfuko wa sandarusi ambapo alipoukaribia na kuugusa alihisi kuwa kuna kitu kizito na baada ya kufungua ndipo alipogundua kuwa ni bunduki.



Anasema kuwa baada ya kugundua kwamba mfuko huo umebeba bunduki iliyotelekezwa aliita watu waliokuwa maeneo ya karibu na kuwaonesha na baadaye kuamua kuwaita Askari Polisi wa kituo cha Kitahana na kuichukua.


No comments: