Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Silima |
SERIKALI ya Tanzania
imewataka wakimbizi wa Burundi
wanaohifadhiwa katika Kambi ya Mtabila wilayani Kasulu mkoani Kigoma, kutumia
vizuri muda uliobaki kuanzia sasa hadi Desemba 31, kujiorodhesha kwa hiari ili
kurudishwa nchini kwao kwa heshima.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Silima
alisema hayo katika Kambi hiyo ya wakimbizi na kuonya kuwa baada ya muda huo
hali itakuwa ngumu kwa wakimbizi hao.
Pia alielezea kutoridhishwa na kasi ndogo ya wakimbizi hao
kujiorodhesha kurudishwa nchini kwao kwa hiari tangu wafutiwe hadhi ya ukimbizi
na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emanuel Nchimbi Agosti mosi mwaka huu
Alisema hadi kufikia Desemba 31 mwaka huu, wakimbizi wote
watarejeshwa kwa hiari na kwa kufuata utaratibu wa Sheria za Kimataifa za
kuwarudisha wakimbizi
Kutokana na hilo ametoa mwito
kwa wakimbizi hao kuliangalia jambo hilo
kwa makini kabla muda haujaisha.
Akisisitiza, Silima alisema baada ya muda huo kupita, hadhi yao itabadilika kwani kwa sasa hawana hadhi ya ukimbizi
waliyokuja nayo na ndiyo maana Tume ya Pande Tatu imeona ni jambo la maana
kuwarudisha wakimbizi hao nchini kwao Burundi.
Alisema wakimbizi hao wanaonekana kupuuza mwito na agizo la
Serikali ya Tanzania
lililotolewa kwa niaba ya Tume ya Pande Tatu la kuwataka kurejea nchini mwao.
Silima alisema tangu wakimbizi hao wafutiwe hadhi ya
ukimbizi hakuna jitihada zozote wanazoonesha za kuunga mkono suala la kurudi
nchini mwao.
Mkuu wa Wilaya Kasulu, Dahn Makanga alisema kusuasua kwa
wakimbizi hao kujiandikisha kurudi nchini mwao kwa hiari, kunaonesha hawataki
kutumia nafasi hiyo kurudi kwa hiari na kwa heshima kama ambavyo Serikali ya Tanzania, Burundi na Shirika la Umoja wa
Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) walikubaliana
No comments:
Post a Comment