Karibu kwenye Blog ya Kijamii ya Kigoma yetu kwa habari na matangazo kwa bei nafuu sana. Tunakalibisha maoni, ushauri na habari zako ili tuijenge Tanzania kwa pamoja.

Thursday, February 9, 2012

Mkakati kusafisha Kigoma Ujiji waanza

Manispaa ya Kigoma Ujiji

HALMASHAURI ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, imeanza utekelezaji wa mkakati wa kuuweka
mji wa Kigoma Ujiji katika mazingira safi baada ya vikundi vya uzoaji taka kuanza kufanya
kazi.

Ofisa Afya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Ernest Nkonyozi alisema hayo juzi wakati akipokea vifaa vya kufanya usafi vilivyotolewa na Mradi wa Maendeleo ya Bonde la Ziwa Tanganyika. Aliongeza kuwa mkakati huo unakusudia kuifanya manispaa hiyo kuwa miongoni mwa manispaa zitakazoongoza kwa usafi.


Pamoja na hilo, Nkonyozi alisema kuwa ofisi yake imeongeza magari ya kuzolea taka kutoka mawili yaliyokuwa awali na kufikia matatu huku magari mawili yakiwa njiani kuongeza nguvu katika mkakati huo.


Kwa sasa alisema kuwa Manispaa ya Kigoma Ujiji bado inakabiliwa na hali mbaya ya taka kutokana na kiasi kikubwa cha taka kinachozalishwa kushindwa kuzolewa. Kwa sasa tani 120 za taka huzalishwa kwa mwezi wakati uwezo wa manispaa hiyo kuzoa taka hizo ni tani 46 ambazo ni chini ya nusu ya kiwango kinachozalishwa.


Nkonyozi alisema tayari juhudi za kuzoa taka zinaonekana kuongezeka kutokana na kuanza kwa vikundi vya kufanya usafi mitaani ambapo taka zote zinazozalishwa huzolewa na kuwekwa kwenye madampo ya muda ambayo yameongezeka na kufikia 40 kutoka 25 ya awali.


Mratibu wa mradi huo, Hawa Mshamu alisema wadau mbalimbali wana jukumu la kuunga mkono na kusaidia mkakati wa kuuweka mji huo katika hali ya usafi. Vifaa vilivyotolewa na mradi huo ni mafagi

No comments: